Yobu 25

Jibu la Bildadi

1 Kisha Bildadi, Mshuhi, akajibu:

2 “Mungu ni mwenye uwezo mkuu,

watu wote na wamche.

Yeye huweka amani mpaka juu kwake mbinguni.

3 Nani awezaye kuhesabu majeshi yake?

Ni nani asiyeangaziwa na mwanga wake?

4 Mtu awezaje basi, kuwa mwadilifu mbele ya Mungu?

Binadamu tu awezaje kujidai kuwa safi?

5 Kwake Mungu, hata mwezi haungai vya kutosha;

nyota nazo si safi mbele yake;

6 sembuse mtu ambaye ni mdudu,

binadamu ambaye ni buu tu!”