Zaburi 114

Mungu na watu wake

1 Watu wa Israeli walipotoka Misri,

wazawa wa Yakobo walipotoka ugenini,

2 Yuda ikawa maskani ya Mungu,

Israeli ikawa milki yake.

3 Bahari iliona hayo ikakimbia;

mto Yordani ukaacha kutiririka!

4 Milima ilirukaruka kama kondoo dume;

vilima vikaruka kama wanakondoo!

5 Ee bahari, imekuwaje hata ukakimbia?

Nawe Yordani, kwa nini ukaacha kutiririka?

6 Enyi milima, mbona mliruka kama kondoo dume?

Nanyi vilima, mmerukaje kama wanakondoo?

7 Tetemeka, ee dunia mbele yake Mwenyezi-Mungu;

tetemeka mbele ya Mungu wa Yakobo,

8 anayeugusa mwamba ukawa bwawa la maji,

nayo majabali yakawa chemchemi za maji!