Zaburi 120

Kuomba msaada

(Wimbo wa Kwenda Juu

)

1 Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,

naye akanijibu.

2 Uniokoe ee Mwenyezi-Mungu,

na watu wadanganyifu na waongo.

3 Enyi watu wadanganyifu, mtapewa kitu gani?

Mtaadhibiwa namna gani?

4 Kwa mishale mikali ya askari,

kwa makaa ya moto mkali!

5 Ole wangu kwamba naishi kama mgeni huko Mesheki;

naishi kama mgeni katika mahema ya Kedari.

6 Nimeishi muda mrefu mno

kati ya watu wanaochukia amani!

7 Wakati ninaposema nataka amani,

wao wanataka tu vita.