Zaburi 125

Usalama wa watu wa Mungu

(Wimbo wa Kwenda Juu)

1 Wanaomtegemea Mwenyezi-Mungu, wako kama mlima Siyoni,

ambao hautikisiki bali wabaki imara daima.

2 Kama Yerusalemu inavyozungukwa na milima,

ndivyo Mwenyezi-Mungu awazungukavyo watu wake,

tangu sasa na hata milele.

3 Waovu hawataendelea kutawala nchi ya waadilifu;

wasije waadilifu nao wakafanya maovu.

4 Ee Mwenyezi-Mungu, uwe mwema kwa watu wema,

kwa wale wanaozitii amri zako.

5 Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya

uwakumbe pamoja na watenda maovu.

Amani iwe na Israeli!