Zaburi 130

Kuomba msaada

(Wimbo wa Kwenda Juu)

1 Toka upeo wa unyonge wangu,

nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.

2 Ee Bwana, sikia sauti yangu,

uitegee sikio sauti ya ombi langu.

3 Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu

nani, ee Bwana, angeweza kusalimika?

4 Lakini kwako twapata msamaha,

ili sisi tukuheshimu.

5 Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote;

nina imani sana na neno lake.

6 Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu

kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko;

kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi.

7 Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,

maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili,

kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa.

8 Yeye atawakomboa watu wa Israeli

kutoka katika maovu yao yote.