Msifuni Mungu
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1 Njoni kumsifu Mwenyezi-Mungu enyi watumishi wake wote,
enyi nyote mnaotumikia usiku nyumbani mwake.
2 Inueni mikono kuelekea mahali patakatifu,
na kumtukuza Mwenyezi-Mungu!
3 Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni;
yeye aliyeumba mbingu na dunia.