Zaburi ya kumsifu Mungu
1 Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mungu katika patakatifu pake;
msifuni katika mbingu zake kuu.
2 Msifuni kwa sababu ya matendo yake makuu;
msifuni kwa ajili ya utukufu wake mkuu.
3 Msifuni kwa mlio wa tarumbeta;
msifuni kwa zeze na kinubi!
4 Msifuni kwa ngoma na kucheza;
msifuni kwa filimbi na banjo!
5 Msifuni kwa kupiga matoazi.
Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.
6 Kila kiumbe hai kimsifu Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!