Wimbo wa ushindi
1 Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya;
msifuni katika kusanyiko la waaminifu!
2 Furahi ee Israeli kwa sababu ya Muumba wako,
wakazi wa Siyoni shangilieni kwa sababu ya Mfalme wenu.
3 Lisifuni jina lake kwa ngoma,
mwimbieni kwa ngoma na zeze.
4 Maana Mwenyezi-Mungu hupendezwa na watu wake;
yeye huwapamba wanyonge kwa ushindi.
5 Watu waaminifu wafurahi kwa fahari;
washangilie hata walalapo.
6 Wabubujike sifa kuu za Mungu,
na panga zenye makali kuwili mikononi mwao,
7 wawalipe kisasi watu wa mataifa,
wawaadhibu watu wasiomjua Mungu;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo,
na viongozi wao kwa pingu za chuma,
9 kusudi watekeleze adhabu iliyoamriwa!
Hiyo ndiyo fahari ya waaminifu wa Mungu.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!