Zaburi 136

Wimbo wa shukrani

1 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

2 Mshukuruni Mungu wa miungu;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

3 Mshukuruni Bwana wa mabwana;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

4 Ndiye peke yake atendaye makuu ya ajabu;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

5 Ndiye aliyeziumba mbingu kwa hekima;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

6 Ndiye aliyeitengeneza nchi juu ya vilindi vya maji;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

7 Ndiye aliyeumba jua, mwezi na nyota;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

8 Jua liutawale mchana;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

9 Mwezi na nyota vitawale usiku;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

10 Ndiye aliyewaua wazaliwa wa kwanza wa Misri;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

11 Akawaondoa watu wa Israeli kutoka huko;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

12 Kwa mkono wake wenye nguvu na enzi;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

13 Ndiye aliyeigawa Bahari ya Shamu sehemu mbili;

kwa maana fadhili zake zadumu milele,

14 akawapitisha watu wa Israeli humo;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

15 Lakini akawazamisha humo Farao na jeshi lake;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

16 Ndiye aliyewaongoza watu wake jangwani;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

17 Ndiye aliyewapiga wafalme wenye nguvu;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

18 Akawaua wafalme maarufu;

kwa maana fadhili zake zadumu milele;

19 akamuua Sihoni, mfalme wa Waamori,

kwa maana fadhili zake zadumu milele;

20 na Ogu, mfalme wa Bashani;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

21 Akachukua nchi zao akawapa watu wake;

kwa maana fadhili zake zadumu milele;

22 ziwe riziki ya Israeli, mtumishi wake;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

23 Ndiye aliyetukumbuka wakati wa unyonge wetu;

kwa maana fadhili zake zadumu milele;

24 akatuokoa kutoka maadui zetu;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

25 Ndiye akipaye kila kiumbe chenye uhai chakula;

kwa maana fadhili zake zadumu milele.

26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni;

kwa maana fadhili zake zadumu milele!