Uzuri wa umoja kati ya watu
(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)
1 Ni jambo zuri na la kupendeza sana
ndugu kuishi pamoja kwa umoja.
2 Ni kama mafuta mazuri yatiririkayo kichwani,
mpaka kwenye ndevu zake Aroni,
mpaka upindoni mwa vazi lake shingoni.
3 Ni kama umande wa mlima Hermoni,
uangukao juu ya vilima vya Siyoni!
Huko Mwenyezi-Mungu ameahidi kuwabariki watu wake,
kuwapa uhai usio na mwisho.