Zaburi 131

Kumtumainia Mungu kwa utulivu

(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)

1 Ee Mwenyezi-Mungu, sina moyo wa kiburi;

mimi si mtu wa majivuno.

Sijishughulishi na mambo makuu,

au yaliyo ya ajabu mno kwangu.

2 Ila nafsi yangu imetulia na kuwa na amani,

kama mtoto mchanga alivyotulia na mama yake;

ndivyo nafsi yangu ilivyo tulivu.

3 Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,

tangu sasa na hata milele.