Zaburi 129

Sala dhidi ya maadui wa Israeli

(Wimbo wa Kwenda Juu)

1 “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu

Kila mtu katika Israeli na aseme:

2 “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu,

lakini hawakufaulu kunishinda.

3 Walinijeruhi vibaya mgongoni mwangu,

wakafanya kama mkulima anayelima shamba.

4 Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu;

amezikata kamba za hao watu waovu.”

5 Na waaibishwe na kurudishwa nyuma,

wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni.

6 Wawe kama nyasi juu ya paa la nyumba,

ambazo hunyauka kabla hazijakua,

7 hakuna anayejishughulisha kuzikusanya,

wala kuzichukua kama matita.

8 Hakuna apitaye karibu atakayewaambia:

“Mwenyezi-Mungu awabariki!

Twawabariki kwa jina la Mwenyezi-Mungu!”