Zaburi 126

Kuomba nguvu mpya

(Wimbo wa Kwenda Juu)

1 Mwenyezi-Mungu alipoturekebisha na kuturudisha Siyoni,

tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!

2 Hapo tuliangua kicheko;

tulishangilia kwa furaha.

Nao watu wa mataifa mengine walisema:

“Mwenyezi-Mungu amewatendea mambo makubwa!”

3 Kweli Mwenyezi-Mungu alitutendea mambo makubwa,

tulifurahi kwelikweli!

4 Ee Mwenyezi-Mungu, urekebishe tena hali yetu,

kama mvua inavyotiririsha maji katika mabonde makavu.

5 Wanaopanda kwa machozi,

watavuna kwa shangwe.

6 Wanaokwenda kupanda mbegu wakilia,

watarudi kwa furaha wakichukua mavuno.